Ticker

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Wizara kutengeneza Database ya Diaspora kwa kushirikiana na IOM

Wizara kutengeneza Database ya Diaspora kwa kushirikiana na IOM

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo akizungumza wakati wa kikao kuhusu uundwaji wa Database na Tovuti kuhusu masuala ya Diaspora. Kikao hicho kiliwashirikisha Wajumbe kutoka Ofisi ya Rais Zanzibar, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uhamiaji na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji hapa nchini (IOM).
Wajumbe kutoka IOM, Ofisi ya Rais Zanzibar na Uhamiaji wakimsikiliza Bibi Jairo (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho
Mwakilishi kutoka IOM, Bi. Mia Immelback akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
Bibi Jairo (wa pili kulia) akiwa na Wajumbe wengine kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Mwakilishi wa IOM (hayupo pichani). Kutoka kushoto ni Bw. Mkumbwa Ally, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasialiano katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Kalumuna, Mkuu wa Kitengo cha ICT, Wizara ya Mambo ya Nje na Bi. Susan kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.
Bw. Kalumuna akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
Picha na Reginald Kisaka.

Post a Comment

0 Comments